Wanachama wa Yanga Wachanga Milioni 5 Kulipia Faini ya Ally Kamwe: Wanachama na mashabiki wa Yanga SC walimtoza faini Ally Kamwe; TFF imemtoza faini ya shilingi milioni 5 kufuatia maamuzi ya Kamati ya Maadili.
Dar es Salaam, Tanzania – Wanachama na mashabiki wa Yanga SC wameonyesha mshikamano mkubwa kwa kuchangia jumla ya shilingi milioni 5 kulipa faini ya afisa habari wa klabu hiyo, Ally Kamwe. Faini hiyo imetolewa na Kamati ya Maadili ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kutokana na makosa aliyokutwa nayo.
Wanachama wa Yanga Wachanga Milioni 5 Kulipia Faini ya Ally Kamwe
Leo Aprili 24, 2025 Ally Kamwe amekabidhiwa rasmi kiasi cha shilingi milioni 5.2 fedha ambazo zitatumika moja kwa moja kulipa faini hiyo kadri itakavyopangwa na mamlaka husika.

Faini ya TFF: Tsh 5,000,000
Fedha zilizochangwa: Tsh 5,289,000
Hatua hiyo imepongezwa na baadhi ya viongozi, mashabiki na wanachama wa klabu hiyo wakieleza kuwa tukio hilo lilikuwa ni kuonyesha mshikamano, upendo wa dhati kwa klabu yao na heshima kwa uongozi unaowawakilisha.
CHECK ALSO:
- Liverpool Karibu Kutwaa Ubingwa wa EPL 2024/25, Baada ya Arsenal Kulazimishwa Sare
- Matokeo JKU vs Singida Black Stars Leo 24/04/2024 Muungano Cup
- Kikosi cha Simba Kilichosafiri Leo Kwenda Afrika Kusini kwa Mchezo vs Stellenbosch
- Kombe la Muungano 2025 Kuchezwa Pemba, ZFF Yahamishia Mechi Uwanja wa GombaniÂ
Weka maoni yako