Pilato wa Simba Beida Apangwa Kuchezesha Mechi ya FIFA Club World Cup 2025 | Shirikisho la Soka Duniani (FIFA) limemteua mwamuzi wa Mauritania, Dahane Beida kuchezesha mchezo wa hatua ya makundi kati ya Inter Milan (Italia) na Urawa Reds (Japan) kwenye michuano ya Kombe la Dunia la Klabu mwaka 2025, itakayochezwa Juni 21, 2025.
Pilato wa Simba Beida Apangwa Kuchezesha Mechi ya FIFA Club World Cup 2025
Inter Milan vs Urawa Reds
- Tarehe: 21 Juni 2025
- Eneo: Marekani
- Ligi: FIFA Club World Cup 2025
- Mwamuzi Mkuu: Dahane Beida 🇲🇷
Kabla ya kuteuliwa na FIFA, kumbukumbu ya mwisho ya Beida barani Afrika ilikuwa ni kati ya Simba SC (Tanzania) na RS Berkane (Morocco) hatua ya pili ya fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika iliyofanyika Mei 2024 kwenye Uwanja wa Amaan, Zanzibar.

Mechi hiyo ilikuwa na mvutano mkubwa, lakini Beida aliichezea kwa ustadi mkubwa, hivyo kupelekea FIFA kumkabidhi majukumu ya hali ya juu ya kimataifa.
Dahane Beida kupewa mchezo wa Inter Milan dhidi ya Urawa Reds ni ishara ya maendeleo ya waamuzi wa Kiafrika na ushahidi wa kazi nzuri aliyofanya katika mechi kama ile ya Simba SC dhidi ya Berkane. Wadau wa soka barani Afrika wana kila sababu ya kujivunia mafanikio haya.
CHECK ALSO:
Weka maoni yako