Himid Mao Mkami Karibu Kujiunga Tena na Azam

Himid Mao Mkami Karibu Kujiunga Tena na Azam, Baada ya Kumaliza Mkataba na Tala’ea El Gaish. KIUNGO wa kimataifa wa Tanzania, Himid Mao Mkami anaripotiwa kuwa katika mazungumzo ya mwisho ya kurejea Azam FC, baada ya kumalizika kwa mkataba wake na Tala’ea El Gaish ya Ligi Kuu ya Misri.

Mao ambaye alicheza vyema Azam FC kabla ya kutimkia kimataifa, anatarajiwa kujiunga na timu hiyo ya Dar es Salaam iwapo makubaliano ya mwisho yatafikiwa. Usajili huo ukikamilika utaimarisha kwa kiasi kikubwa safu ya kiungo ya Azam FC kuelekea msimu ujao wa mashindano ya ndani na nje ya nchi.

Himid Mao Mkami Karibu Kujiunga Tena na Azam
Himid Mao Mkami Karibu Kujiunga Tena na Azam

Iwapo atasajiliwa, Himid Mao atakuwa miongoni mwa wachezaji wapya waliothibitishwa kuichezea Azam FC msimu huu, akiwemo kipa mahiri Aishi Manula, pamoja na chipukizi Muhsini Malima na Lameck Lawi. Hii inadhihirisha kuwa Azam FC imejipanga vyema kwa ajili ya msimu wa 2025/2026, huku ikiboresha kikosi mapema.

CHECK ALSO:

  1. Diogo Jota Afariki Dunia kwa Ajali ya Barabarani Akiwa na Umri wa Miaka 28
  2. Miloud Hamdi Ajiunga na Ismaily SC ya Misri
  3. Tanzania Prisons Yajihakikishia Kubaki Ligi Kuu NBC 2025/2026
  4. Play Off Tanzania Prisons vs Fountain Gate Leo Juni 30, Nani Kusalia Ligi Kuu?