Zawadi ya Mashindano ya CAF CHAN 2024/2025

Zawadi ya Mashindano ya CAF CHAN 2024/2025: SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetangaza rasmi ongezeko kubwa la fedha za zawadi kwa ajili ya michuano ya CHAN 2024 (Michuano ya Mataifa ya Afrika). Hatua hii inalenga kuongeza uelewa wa mashindano hayo na kuhimiza ushiriki wa wachezaji wa ndani kutoka nchi za Afrika.

Katika tangazo hili jipya, CAF imeweka rekodi mpya ya fedha za zawadi, na faida za kifedha kwa timu zote shiriki, kutoka kwa wale waliotolewa katika hatua ya makundi hadi mabingwa wa michuano hiyo.

Zawadi ya Mashindano ya CAF CHAN 2024/2025

Zawadi ya Mashindano ya CAF CHAN 2024/2025
Zawadi ya Mashindano ya CAF CHAN 2024/2025
Nafasi Zawadi (USD)
🏆 Mabingwa $3,500,000
🥈 Washindi wa Pili $1,200,000
🥉 Nafasi ya Tatu $700,000
🏅 Nafasi ya Nne $600,000
🎯 Robo Fainali $450,000 kila timu
Nafasi ya 3 (Makundi) $300,000 kila timu
⚠️ Nafasi ya 4 (Makundi) $200,000 kila timu
🔚 Nafasi ya 5 (Kundi la timu 5) $200,000

Ongezeko hili ni kubwa ikilinganishwa na matoleo ya awali ya CHAN, na linaonyesha dhamira ya dhati ya Rais wa CAF, Dk. Patrice Motsepe katika kuongeza thamani ya mashindano ya CHAN na kuyaweka kwenye ramani ya michuano bora zaidi barani Afrika.

CHECK ALSO:

  1. Wachezaji wa Kigeni Ndani ya Simba SC 2025/2026
  2. Mbeya City FC Yafanya Maboresho ya Kikosi, Yawaaga Wachezaji 9 na Kusajili 3
  3. JKT Tanzania Yaachana na Wachezaji 7, Dirisha Kubwa La Usajili 2025/26
  4. Mashujaa FC Wameachana na Wachezaji 10 Kuelekea Ligi Kuu Bara 2025/2026