Andy Boyeli Ajiunga Rasmi na Yanga kwa Msimu Mpya 2025/2026: MSHAMBULIAJI mpya wa Young Africans (Yanga SC) ya Tanzania, Andy Boyeli, kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (🇨🇩), amewasili rasmi jijini Dar es Salaam kuanza maandalizi ya msimu mpya wa Ligi Kuu ya NBC 2025/2026.
Andy Boyeli Ajiunga Rasmi na Yanga kwa Msimu Mpya 2025/2026
Boyeli ambaye hivi karibuni alitambulishwa kuwa miongoni mwa wachezaji wapya wa klabu ya Yanga SC, anatarajiwa kuungana na wachezaji wenzake kwenye kambi ya timu hiyo ikijiandaa na michuano ya ndani na nje ya nchi ikiwemo Ligi ya Mabingwa Afrika.

Usajili wa Andy Boyeli unaonekana kuwa sehemu ya mikakati ya klabu hiyo kuimarisha safu yake ya ushambuliaji hasa kufuatia kuondokewa na washambuliaji kadhaa waliokuwa sehemu ya kikosi hicho msimu uliopita. Boyeli amefanya vyema kwenye ligi ya Kongo na mashindano ya CAF, hivyo kuwapa matumaini makubwa mashabiki wa Yanga kwa msimu ujao.
Kwa kuwasili kwa Andy Boyeli, Young Africans wanaendelea kudhihirisha dhamira yao ya kutetea mataji yao na kufanya vyema katika mashindano ya Afrika. Mashabiki wa Yanga wana hamu ya kumuona mshambuliaji huyo mpya akionyesha ubora wake mwanzoni mwa msimu mpya.
CHECK ALSO:
Weka maoni yako