Matokeo ya Simba Vs Al Zulfi Leo 20/08/2025 Pre Season: Simba SC vs Al Zulfi Leo Saa 11:30 Jioni | Mchezo wa Kimataifa wa Kirafiki Saudi Arabia.
Klabu ya Simba SC ya Tanzania inatarajiwa kushuka dimbani leo saa 11:30 Jioni kwa ajili ya mchezo wa kirafiki wa kimataifa dhidi ya Al Zulfi FC ya Saudi Arabia. Mechi hii ni sehemu ya maandalizi ya timu kwa ajili ya msimu mpya wa mashindano ya ndani na nje ya nchi.
Simba SC imekuwa ikitumia fursa ya mechi za kirafiki nje ya nchi kuongeza uzoefu wa wachezaji wake na kuimarisha muunganiko wa kikosi kipya kwa ajili ya msimu ujao. Mechi dhidi ya Al Zulfi inatarajiwa kutoa nafasi kwa wakufunzi hao kuwapima ujuzi wachezaji wapya na wakongwe, pamoja na kujaribu mbinu mbalimbali za kiufundi.
Kwa Al Zulfi, hii ni mechi ya heshima na majaribio, huku wakichukua fursa hiyo kuonyesha ujuzi wao dhidi ya moja ya klabu kubwa barani Afrika.
Matokeo ya Simba Vs Al Zulfi Leo 20/08/2025 Pre Season
πΉπΏ SIMBA SC 1-0 Al ZULFI πΈπ¦
- FT: SIMBA 1-0 ZULFI, Ushindi kwenye mchezo wa kirafiki kwa Simba
- Jean Charles Ahoua anapiga faulo inayaomshinda kipa wa timu pinzani

Maandalizi ya Kimataifa: Simba SC inatarajia kujidhihirisha kimataifa kabla ya michuano ya CAF na Ligi Kuu ya Tanzania Bara.
Fursa kwa Wachezaji Wapya: Mechi ya kirafiki ni fursa nzuri kwa nyota wanaochipukia kuonyesha ujuzi wao mbele ya wakufunzi.
SOMA PIA:
Weka maoni yako