MATOKEO ya Taifa Stars Leo Vs Morocco 22/08/2025, TIMU ya soka ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars, itashuka dimbani leo kwa mara ya kwanza katika mchezo muhimu wa robo fainali ya michuano ya Mataifa ya Afrika (CHAN 2025) dhidi ya Morocco. Mchezo huu wa kusisimua utapigwa kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam, kuanzia saa 2:00 Usiku.
Kwa mara nyingine, Taifa Stars imeweka matumaini ya Watanzania wote mikononi mwao, kufuatia kuonyesha kiwango kikubwa katika hatua ya makundi na kufuzu kwa robo fainali. Ushindi katika mechi ya leo utaifanya Tanzania kufuzu kwa hatua ya nusu fainali, hivyo kuashiria historia kubwa kwa soka la taifa.
Kwa upande wake, Morocco imekuwa na rekodi kubwa katika michuano ya CHAN, ikiwa ni miongoni mwa washindani wakuu wa taji hilo. Hii ina maana kwamba Stars italazimika kushindana kwa kiwango cha juu ili kupata matokeo chanya mbele ya mashabiki wao.
MATOKEO ya Taifa Stars Leo Vs Morocco 22/08/2025
FTÂ |Â TANZANIAÂ Â Â 0-1Â Â Â MOROCCO

SOMA PIA:
Weka maoni yako