KMKM Yashinda Ngao ya Jamii Zanzibar 2025

KMKM Yashinda Ngao ya Jamii Zanzibar 2025, KMKM Yatwaa Ngao ya Jamii Zanzibar 2025 Baada ya Kuibuka na Ushindi Dhidi ya Mlandege FC kwa Penati.

KMKM Yashinda Ngao ya Jamii Zanzibar 2025

KMKM SC imetwaa Ngao ya Jamii ya Zanzibar 2025 baada ya kuifunga Mlandege FC mabao 5-3 kwa mikwaju ya penalti. Mchezo huo uliopigwa visiwani Zanzibar, ulimalizika kwa sare ya bila kufungana baada ya dakika 90, matokeo yakiwa 0-0.

Mechi hiyo ilikuwa ngumu, huku KMKM na Mlandege zikionyesha nidhamu bora ya ulinzi. Licha ya mashambulizi ya hapa na pale, hakuna timu iliyofanikiwa kupata bao katika muda wa kawaida, hivyo kulazimisha mechi hiyo kuamuliwa kwa mikwaju ya penalti.

KMKM Yashinda Ngao ya Jamii Zanzibar 2025
KMKM Yashinda Ngao ya Jamii Zanzibar 2025

Katika mikwaju ya penalti, KMKM walionyesha utulivu mkubwa na kufanikiwa kufunga mabao matano kwa matatu ya wapinzani wao, hivyo kufanikiwa kutwaa ubingwa.

Ngao ya Jamii Zanzibar ni mashindano maalum yanayowakutanisha vinara wa ligi na washindi wa kombe la FA na kuashiria kuanza rasmi kwa msimu mpya wa soka visiwani Zanzibar. Ushindi huo wa KMKM umewapa heshima ya kuanza msimu na ubingwa na kuendeleza historia yao katika soka la visiwani.

CHECK ALSO:

  1. Manchester Derby, Imeisha kwa Man City 3-0 Man United
  2. Yanga vs Simba Leo Saa Ngapi 16/09/2025
  3. Matokeo ya Yanga vs Simba Leo 16/09/2025
  4. Viingilio Ngao ya Jamii 2025, Yanga vs Simba 16/9/2025