Jezi Mpya za Yanga za Kimataifa CAF 2025/2026, Yanga SC Kutambulisha Jezi Mpya za CAF Champions League Wiki Hii Kabla ya Mchezo wa Kwanza Zanzibar.
Klabu ya Yanga SC inatarajiwa kutambulisha jezi zake mpya za michezo ya kimataifa ya CAF Champions League mapema wiki hii, ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya mchezo wao wa kwanza wa hatua ya makundi utakaochezwa Novemba 22 katika Uwanja wa Amaan, Zanzibar.
Hatua hii inalenga kuwapa mashabiki muda wa kutosha kujipatia jezi hizo mpya kabla ya siku ya mchezo, ili kuonyesha mshikamano na kuipa nguvu timu yao katika safari ya kimataifa. Uongozi wa Yanga SC umedai kuwa jezi hizo zimebuniwa kwa ubora wa juu, zikibeba ubunifu unaoendana na hadhi ya klabu hiyo kongwe barani Afrika.
Jezi mpya zinatarajiwa kubeba alama za kipekee zinazoakisi utambulisho wa Yanga SC pamoja na kaulimbiu ya msimu huu wa mashindano ya CAF. Mashabiki wengi wameshaonyesha hamu kubwa ya kuziona na kuzivaa jezi hizo, wakiamini zitakuwa alama ya utambulisho na fahari ya timu yao katika michuano ya kimataifa.
Jezi Mpya za Yanga za Kimataifa CAF 2025/2026


Yanga SC itaanza kampeni zake za CAF Champions League kwa mchezo muhimu dhidi ya AS FAR ya Morocco, ambapo mashabiki wanatarajiwa kujitokeza kwa wingi visiwani Zanzibar kuisapoti timu yao.
Kwa sasa, maandalizi yanaendelea kwa kasi, na uzinduzi wa jezi hizo unatarajiwa kuwa moja ya matukio makubwa yatakayozungumziwa zaidi na wapenzi wa soka nchini Tanzania wiki hii.
CHECK ALSO:








Weka maoni yako