Kikosi cha Al Ahly Kilichosafiri Kuivaa Yanga: Al Ahly yatangaza kikosi cha safari kuelekea Zanzibar.
Klabu bingwa wa Afrika, Al Ahly SC ya Misri, imetangaza rasmi kikosi chake cha wachezaji kitakachosafiri kwenda Zanzibar kwa ajili ya mchezo wa CAF Champions League, Hatua ya Makundi – Mechi ya Nne, dhidi ya Young Africans SC (Yanga).
Taarifa hiyo imetolewa asubuhi hii, ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya mwisho kabla ya mchezo huo muhimu unaotarajiwa kuchezwa katika mazingira ya ushindani mkubwa, kutokana na nafasi ya kila timu kwenye msimamo wa kundi.
Kikosi cha Al Ahly Kilichosafiri Kuivaa Yanga

Orodha ya wachezaji waliosafiri wa Al Ahly:-
- El Shenawy
- Shobeir
- Hamza
- Yassin
- Beckham
- Ben Romdhane
- Yasser
- Trezeguet
- Sherif
- Shoukry
- Attia
- El Shahhat
- Bencharki
- Belammari
- Emam
- Dieng
- Ahmed Eid
- Zizo
- El Gazar
- Othman
- Taher
- Hany
- Koka
Kikosi hicho kina mchanganyiko wa wachezaji wenye uzoefu mkubwa wa michuano ya CAF pamoja na vijana wenye nguvu, jambo linaloonyesha dhamira ya Al Ahly kupambana vikali katika mchezo huo.
CHECK ALSO:






Weka maoni yako