CAF Confederation Cup 2025/26 Azam FC, Singida Black Stars na KMKM

CAF Confederation Cup 2025/26 Azam FC, Singida Black Stars na KMKM: Wawakilishi wa Tanzania Bara na Zanzibar katika msimu wa 2025/26 CAF Confederation Cup (CAFCC) wametangaza wapinzani wao katika hatua ya awali ya michuano hiyo kufuatia droo rasmi.

CAF Confederation Cup 2025/26 Azam FC, Singida Black Stars na KMKM

Azam FC, moja ya timu zilizotamba zaidi kwenye Ligi Kuu Bara, itamenyana na Al Merriekh Bentiu ya Sudan Kusini. Wakati huohuo, Singida Black Stars itamenyana na Rayon Sports ya Rwanda. Wawakilishi wa Zanzibar, KMKM, watamenyana na AS Sport ya Djibouti.

Kwa mujibu wa kalenda ya CAF, mechi za mkondo wa kwanza zitachezwa ugenini kati ya Septemba 19 na 21, 2025, na mechi za mkondo wa pili zitachezwa nyumbani kati ya Septemba 26 na 28, 2025.

CAF Confederation Cup 2025/26 Azam FC, Singida Black Stars na KMKM
CAF Confederation Cup 2025/26 Azam FC, Singida Black Stars na KMKM

Katika raundi inayofuata, mshindi wa mchezo kati ya Azam FC na Al Merriekh Bentiu atamenyana na mshindi wa mechi kati ya KMKM na AS Sport, huku mshindi wa mchezo kati ya Singida Black Stars na Rayon Sports akichuana na mshindi wa mchezo kati ya Flambeau Du Centre ya Burundi na timu kutoka Libya itakayojulikana baadaye.

Mechi za Hatua ya Awali CAFCC 2025/26 kwa Wawakilishi wa Tanzania:

  • πŸ‡ΈπŸ‡Έ Al Merriekh Bentiu πŸ†š πŸ‡ΉπŸ‡Ώ Azam FC

  • πŸ‡·πŸ‡Ό Rayon Sports πŸ†š πŸ‡ΉπŸ‡Ώ Singida Black Stars

  • πŸ‡©πŸ‡― AS Sport πŸ†š πŸ‡ΉπŸ‡Ώ KMKM (Zanzibar)

CHECK ALSO:

  1. Taifa Stars Yatinga Hatua ya Robo Fainali CHAN 2024
  2. Makundi ya Droo ya Kombe la Shirikisho la CAF 2025/26
  3. RATIBA ya CAF Ligi ya Mabingwa Afrika 2025/2026
  4. Makundi ya Droo Ligi ya Mabingwa Afrika CAF 2025/26