CV ya Lassine Kouma Mchezaji Mpya wa Yanga 2025/2026, Lassine Kouma Kutua Yanga, Simba SC Wajiondoa: Katika habari za hivi punde kutoka soko la kimataifa la usajili, klabu ya Simba Sports Club imethibitisha kujitoa katika mbio za kumsajili kiungo wa kati wa Mali Lassine Kouma mwenye umri wa miaka 21. Kwa mujibu wa vyanzo vya habari vya klabu hiyo, hakutakuwa na majadiliano zaidi kati ya Simba na mchezaji huyo.
Uamuzi huo umekuja wakati mahasimu wao, Young Africans SC (Yanga), wakikaribia kukamilisha usajili wa mchezaji huyo ambaye kwa sasa anatajwa kuwa miongoni mwa viungo wa kizazi kipya mwenye kipaji na uwezo mkubwa.
Lassine Kouma ni kiungo mwenye uwezo wa kucheza kama mchezeshaji wa kati (central midfielder) na kiungo wa ushambuliaji. Ana asili ya taifa la Mali 🇲🇱 na ameonyesha kiwango bora katika michuano ya vijana na ligi kuu nchini kwake.
CV ya Lassine Kouma Mchezaji Mpya wa Yanga 2025/2026
Kijana huyo mwenye umri wa miaka 21, ameonyesha uwezo mkubwa wa kupiga pasi za mwisho (key passes), kusoma mchezo, na kuhimili presha katika maeneo ya kati—sifa ambazo zimekuwa kivutio kwa klabu mbalimbali ndani ya Afrika Mashariki.

Date of birth/Age: May 19, 2004 (21)
Citizenship: Mali
Position: Midfield – Attacking Midfield
Current club: Yanga SC
Forma Club: Stade Malien
Joined: 18 July 2025
Contract expires: 17 July 2027
CHECK ALSO:
Weka maoni yako