Kikosi cha Yanga Leo vs JKT Tanzania 18/05/2025: Young Africans Sport Club itamenyana na JKT Tanzania kuanzia tarehe 18 Mei 2025 saa 15:30. Mechi hiyo ni sehemu ya Kombe la Shirikisho.
Mara ya mwisho miamba hawa wawili walikutana katika mchezo wa ligi uliopigwa kwenye Uwanja wa Isahmuyo, baada ya dakika 90 ubao ulisomeka JKT Tanzania 0-0 Yanga SC. Walishiriki pointi moja kila mmoja. Ni wazi JKT Tanzania ndiyo timu pekee iliyopata pointi moja mbele ya Yanga SC kwani baada ya hapo katika mechi zilizofuata Yanga SC haikutoka sare tena kwenye ligi.
Mechi hiyo ilichezwa Februari 10, 2025. Rekodi zinaonyesha kuwa jumla ya dakika 9 ziliongezwa, na dakika tatu ziliongezwa katika kipindi cha kwanza na dakika sita katika kipindi cha pili.
JKT Tanzania kupitia kwa afisa habari wake, Masau Bwire, imesema lengo lake kubwa ni kupata ushindi dhidi ya Yanga SC, kwani ina timu imara na yenye ushindani na lengo lake ni kutwaa ubingwa.
Kikosi cha Yanga Leo vs JKT Tanzania 18/05/2025
Kikosi cha Yanga kinachoaza leo cha Wananchi dhidi ya JKT Tanzania:
- DIARRA
- JOB
- MWENDA
- KIBWANA
- BACCA
- ABUYA
- MUDATHIR
- AZIZ KI
- MAXI
- DUBE
- MZIZE

CHECK ALSO:
Weka maoni yako