Makundi ya Mapinduzi Cup 2025/2026

Makundi ya Mapinduzi Cup 2025/2026 | MAPINDUZI CUP 2026: Makundi na Viwanja Rasmi vya Mashindano.

Makundi ya Mapinduzi Cup 2025/2026

Mashindano ya Mapinduzi Cup 2026 yamepangwa rasmi kuanza tarehe 28 Desemba 2025 na yanatarajiwa kumalizika tarehe 13 Januari 2026. Michuano hii ni sehemu muhimu ya kalenda ya soka Tanzania, ikiwaleta pamoja vilabu vikubwa vya Tanzania Bara na Zanzibar, pamoja na taasisi za kijeshi.

Makundi

Mapinduzi Cup 2026 imeundwa kwa makundi matatu, kila kundi likiwa na timu tatu hadi nne kama ifuatavyo:

Kundi A

  • Mlandege FC
  • Azam FC
  • Singida Black Stars
  • Ura FC

Kundi B

  • Simba SC
  • Muembe Makumbi City
  • Fufuni SC

Kundi C

  • Yanga SC
  • KVZ
  • TRA

Timu zitacheza hatua ya makundi kabla ya kuingia hatua ya nusu fainali na fainali.

Makundi ya Mapinduzi Cup 2025/2026
Makundi ya Mapinduzi Cup 2025/2026

Viwanja Vitakavyotumika

Mashindano yote yatafanyika Zanzibar katika viwanja viwili rasmi:

  • Uwanja wa Amaan, Unguja

  • Uwanja wa Gombani, Pemba

Hatua kubwa ya makundi na nusu fainali zitachezwa Amaan Stadium, huku fainali ikipangwa kuchezwa Gombani Stadium.

CHECK ALSO:

  1. Ratiba ya Mapinduzi Cup 2026
  2. Hassan Mwakinyo vs Stanley Eribo, Boxing Day Disemba 26
  3. Vilabu Vilivyojiunga na African Club Association ACA
  4. CV ya Steve Barker Kocha Mpya wa Simba