Mohammed Bajaber Asaini Mkataba wa Miaka Miwili na Simba SC: Simba SC imekamilisha usajili wa kiungo mshambuliaji na winga Mohammed Bajaber kwa mkataba wa miaka miwili. Klabu hiyo imetangaza rasmi usajili huu na kuongeza Bajaber kwenye kikosi cha wekundu wa msimbazi Simba kuelekea msimu mpya wa mashindano ya ndani na nje ya nchi.
Mohammed Bajaber Asaini Mkataba wa Miaka Miwili na Simba SC
Bajaber anayesifika kwa kasi, uwezo wa kupiga pasi za kumalizia, na ufundi bora uwanjani, ni miongoni mwa wachezaji wapya wanaotarajiwa kuimarisha safu ya ushambuliaji ya Simba SC msimu wa 2025/2026.
Hata hivyo, kutokana na usajili huu rasmi, Bajaber haitastahili kushiriki michuano ya CHAN (Michuano ya Mataifa ya Afrika), ambayo inajumuisha wachezaji wanaoshiriki ligi za ndani za nchi zao pekee. Kujumuishwa kwake katika klabu ya kimataifa kama Simba kunamuondoa kwenye orodha ya wachezaji wanaokidhi vigezo vya CAF kwa mashindano hayo.

Usajili wa Bajaber ni juhudi za Simba kuimarisha kikosi chake kwa ajili ya Ligi Kuu Tanzania Bara, Kombe la Shirikisho la Azam, na Ligi ya Mabingwa Afrika (CAF Champions League). Simba SC inaendelea kudhihirisha dhamira yake ya kuwania mataji yote kwa kuongeza wachezaji wa hali ya juu.
CHECK ALSO:
Weka maoni yako