Ratiba ya Mechi za Ligi ya Mabingwa Ulaya Leo, Michuano ya UEFA Champions League inaendelea tena usiku wa kuamkia leo kwa michezo mingi ya kusisimua inayotarajiwa katika viwanja mbalimbali barani Ulaya.
Moja ya mechi za kusisimua zaidi itakuwa Manchester City dhidi ya Napoli kwenye Uwanja wa Etihad, kuanzia saa 4:00 Usiku (10:00 PM EAT). Katika mechi hii, mchezaji wa zamani wa City Kevin De Bruyne, ambaye sasa ni mchezaji wa Napoli, ataungana na timu yake ya zamani kwa mara ya kwanza. Wachezaji wa zamani wa Manchester United Scott McTominay na Rasmus Højlund pia wanarejea Manchester kama sehemu ya kikosi cha Napoli kinachonolewa na Antonio Conte.
Mechi nyingine ya kuvutia itakuwa Newcastle United dhidi ya Barcelona katika uwanja wa St. James’ Park. Mashabiki watamshuhudia Marcus Rashford akirejea Uingereza baada ya kuondoka Manchester United na kujiunga na Barcelona.

Ratiba ya Mechi za Ligi ya Mabingwa Ulaya Leo
22:00 Man City 🏴 vs 🇮🇹 Napoli
🏟️ Etihad
22:00 Newcastle 🏴 vs 🇪🇸 Barcelona
🏟️ St. James’ Park
22:00 Sporting CP 🇵🇹 vs 🇰🇿 Kairat Almaty
🏟️ José Alvalade, Lisbon
22:00 Eintracht Frankfurt 🇩🇪 vs 🇹🇷 Galatasaray
🏟️ Deutsche Bank Park
CHECK ALSO:








Weka maoni yako