Ratiba ya Vilabu vya Tanzania katika Mashindano ya Kimataifa: Msimu wa kimataifa wa soka unaanza rasmi Jumanne Septemba 16, 2025 kwa mtanange kati ya mahasimu wa jadi, Yanga SC na Simba SC katika mchezo wa Ngao ya Jamii, utakaochezwa kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa kuanzia saa 11:00 jioni.
Mechi hii itaanza msimu mpya wa mashindano ya ndani ya Tanzania kabla ya vilabu hivi vikubwa kushiriki Ligi ya Mabingwa Afrika na Kombe la Shirikisho la CAF.
Ratiba ya Vilabu vya Tanzania katika Mashindano ya Kimataifa
Ngao ya Jamii – Kariakoo Derby
Yanga SC vs Simba SC
- Tarehe: Jumanne, 16 Septemba 2025
- Saa: 11:00 Jioni
- Uwanja: Benjamin Mkapa, Dar es Salaam
CAF Champions League
Wiliete (Angola) vs Yanga SC
- Tarehe: Ijumaa, 19 Septemba 2025
- Saa: 12:00 Jioni
Gaborone United (Botswana) vs Simba SC
- Tarehe: Jumamosi, 20 Septemba 2025
- Saa: 2:00 Usiku

CAF Confederation Cup
El Merriekh Bentiu (Sudan Kusini) vs Azam FC
- Tarehe: Jumamosi, 20 Septemba 2025
- Saa: 11:00 Jioni
Rayon Sports (Rwanda) vs Singida BS
- Tarehe: Jumamosi, 20 Septemba 2025
- Saa: 12:00 Jioni
Mashabiki wa soka Tanzania wanatarajiwa kushuhudia wiki moja ya burudani kali, kwa kuanzia na Ngao ya Jamii kati ya Simba na Yanga, ikifuatiwa na mfululizo wa mechi za kimataifa ambazo klabu za Tanzania zitakuwa na jukumu la kupeperusha bendera ya Taifa katika michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika CAF na Kombe la Shirikisho Afrika.
CHECK ALSO:
Weka maoni yako