Simba Kwenye Mazungumzoni na Singida Black Stars Kumsajili Sowah

Simba Kwenye Mazungumzoni na Singida Black Stars Kumsajili Sowah: Klabu ya Simba Sports Club ya Tanzania imeanza rasmi mazungumzo na klabu ya Singida Black Stars ili kukamilisha usajili wa mshambuliaji wa Ghana Jonathan Sowah mwenye umri wa miaka 26.

Simba Kwenye Mazungumzoni na Singida Black Stars Kumsajili Sowah

Kwa mujibu wa taarifa za ndani ya klabu hiyo, tayari mambo binafsi kati ya mchezaji huyo na Simba SC yameshafanyika kwa mafanikio. Hii inaashiria kuwa hatua inayofuata ni kwa klabu zote mbili kufikia makubaliano juu ya ada ya uhamisho.

Jonathan Sowah anafahamika kwa uwezo wake wa kupachika mabao, kasi na nguvu, na amekuwa mmoja wa wachezaji wanaozungumziwa sana katika soko la uhamisho wa wachezaji msimu huu kutokana na kufanya vyema akiwa na klabu ya Singida Black Stars.

Simba Kwenye Mazungumzoni na Singida Black Stars Kumsajili Sowah
Simba Kwenye Mazungumzoni na Singida Black Stars Kumsajili Sowah

Endapo mazungumzo yatafanikiwa, usajili huu utaimarisha safu ya ushambuliaji ya Simba SC yenye lengo la kuimarika katika mashindano ya ndani na nje ya nchi msimu wa 2025/2026.

Endapo Simba SC itafanikiwa kumsajili Jonathan Sowah, itakuwa ni hatua kubwa katika kujenga kikosi imara chenye ushindani wa hali ya juu. Mashabiki wa klabu hiyo wanatarajiwa kuendelea kufuatilia kwa karibu mchakato huu muhimu wa usajili.

CHECK ALSO:

  1. CV ya Alassane Kanté Mchezaji Mpya wa Simba 2025/2026
  2. Simba Kunasa Kiungo Msenegali Alassane Kanté
  3. Kenya Yajiondoa CECAFA ya Arusha, Yarejea Kujiandaa na CHAN 2024
  4. Mohamed Hussein Avutiwa na Ofa ya Yanga, Usajili Mnono