TETESI za Usajili wa Simba SC 2025/26 Dirisha Dogo | Wachezaji waliosajiliwa na Simba kwenye dirisha dogo la usajili 2025/2026.
Mpaka sasa baada ya dirisha dogo la usajili la msimu wa 2025/2026 kufunguliwa, yapo majina yanayotajwa kutua kwenye kikosi cha Simba kuongeza nguvu na kuipambania nembo ya wanasimba.
Usajili wa Simba SC 2025/26 Dirisha Dogo
Haya hapa baadhi ya majina yanayoitajika kutua kwenye kikosi cha Simba kwenye dirisha dogo la usajili:-

01. James Akamingo
Kiungo mkabaji wa Azam raia wa Ghana James Akamingo(30) ni zaidi ya asilimia 70 msimu ujao atacheza kariakoo derby ✍️… vyanzo vyetu vipo ndani yao Mwamba anawindwa kwa ukaribu zaidi na klabu ya Simba ya Tanzania.
02. KHADIM DIAW
Inaelezwa klabu ya SIMBA SC imeanza mazungumzo na beki wa zamani wa AL-HILAL OMDURMAN, KHADIM DIAW (27) kwa ajili ya kumsajili katika dirisha dogo la usajili mwezi Januari 2026.
Tetesi zilizopo ni kwamba DIAW amepokea ofa kutoka klabu tatu barani Afrika ambazo ni SIMBA SC, USM ALGER na JS KABYLIE ya ALGERIA…. KHADIM DIAW, ambaye aliwahi kuchezea HOROYA AC na AL-HILAL OMDURMAN, kwa sasa ni mchezaji huru anayeweza kusajiliwa bila vikwazo vyovyote…. Timu itayoweka pesa nzuri kwa DIAW basi uhakika wa kupata huduma yake utakua mkubwa…..✍🏾
03. Dramane Kamagate
Dramane Kamagate (20) nyota raia wa Ivory Coast anayekipiga kwenye klabu ya San Pedro ya huko huko kwao Ivory Coast. Dramane ni mshambuliaji wa kati na moja ya sifa zake ni speed na uhatari mbele ya lango la wapinzani.🔥
Msimu uliopita aliibuka kinara wa ufungaji kwenye ligi ya Ivory Coast (Ligue 1) akifunga jumla ya mabao 11. Na kwenye mechi 5 za mwisho msimu huu amefunga jumla ya goli 5.🔥
CHECK ALSO:








Weka maoni yako