Emmanuel Okwi Astaafu Soka la Kulipwa Kimataifa

Emmanuel Okwi Astaafu Soka la Kulipwa Kimataifa na Timu ya Uganda ‘The Cranes’. MSHAMBULIAJI wa zamani wa Simba SC, Yanga SC, na timu ya Taifa ya Uganda “The Cranes,” Emmanuel Arnold Okwi, ametangaza rasmi kustaafu kucheza soka la kimataifa akiwa na umri wa miaka 32. Hatua hii inahitimisha safari yake ya miaka 16 na timu ya taifa ya Uganda.

Kwa sasa Okwi anachezea klabu ya Kiyovu SC ya Rwanda. Alianza kuitumikia nchi yake mwaka 2009, ambapo alifunga mabao 28 katika mechi 95 alizoichezea Uganda. Mnamo 2021, alichukua kama nahodha wa Cranes kufuatia kustaafu kwa nahodha wa zamani, kipa Denis Onyango.

Emmanuel Okwi Astaafu Soka la Kulipwa Kimataifa

Katika ujumbe wake wa kuaga, Okwi aliandika:
“Kuiwakilisha nchi yangu kwenye jukwaa la kimataifa imekuwa ndoto yangu ambayo imetimia kila mara iliacha hisia maalum, na kuwa nahodha wa timu yetu ilikuwa fursa na heshima kubwa.”

Emmanuel Okwi Astaafu Soka la Kulipwa Kimataifa
Emmanuel Okwi Astaafu Soka la Kulipwa Kimataifa

Kustaafu kwa Okwi kunahitimisha muda wake wa kuwa mmoja wa washambuliaji bora waliowahi kuitumikia Uganda, huku akiacha historia ya mchango wake mkubwa kwa taifa katika mashindano ya kimataifa.

CHECK ALSO: