Shirikisho la Soka Afrika CAF Limetoa Orodha ya Vilabu Bora 2025: SHIRIKISHO la Soka barani Afrika (CAF) limetoa orodha yake rasmi ya vilabu bora zaidi barani 2025, ikionyesha mabadiliko makubwa katika nafasi za timu kutokana na mafanikio yao katika mashindano ya kimataifa na ya ndani.
Kwa mujibu wa orodha hiyo, Al Ahly SC ya Misri imesalia katika nafasi ya kwanza ikiwa na pointi 78, ikifuatiwa na Mamelodi Sundowns ya Afrika Kusini yenye pointi 62. Espérance Sportive de Tunis ya Tunisia inashikilia nafasi ya tatu kwa pointi 57.
RS Berkane ya Morocco ipo nafasi ya nne (pointi 52), huku Simba SC ya Tanzania ikiweka historia ya kusalia kwenye nafasi ya tano barani Afrika ikiwa na pointi 48, ikizipita klabu nyingi za bara hilo. Hii ni mara ya kwanza kwa Simba kuingia tano bora ndani ya muda mrefu, ishara ya maendeleo ya soka la Tanzania.
Timu nyingine ya Tanzania, Young Africans SC (Yanga), ipo katika nafasi ya 12 ikiwa na pointi 33, hivyo kudhihirisha nguvu yake katika mashindano ya CAF, hasa Ligi ya Mabingwa na Kombe la Shirikisho/Shirikisho la Soka Afrika CAF Limetoa Orodha ya Vilabu Bora 2025.
Shirikisho la Soka Afrika CAF Limetoa Orodha ya Vilabu Bora 2025

Vilabu 15 Bora CAF 2025
-
Al Ahly SC – 78 pts
-
Mamelodi Sundowns – 62 pts
-
Espérance de Tunis – 57 pts
-
RS Berkane – 52 pts
-
Simba SC – 48 pts
-
Pyramids FC – 47 pts
-
Zamalek SC – 43 pts
-
Wydad AC – 39 pts
-
USM Alger – 39 pts
-
CR Belouizdad – 37 pts
-
Al Hilal SC – 34 pts
-
Young Africans SC – 33 pts
-
ASEC Mimosas – 33 pts
-
TP Mazembe – 30.5 pts
-
Orlando Pirates – 30 pts
CHECK ALSO:
Weka maoni yako