Fursa Mpya za Ajira Air Tanzania Septemba 2024

Fursa Mpya za Ajira Air Tanzania Septemba 2024

Air Tanzania Company Limited (ATCL) imetangaza fursa mpya za ajira kwa watanzania na wageni katika nafasi mbalimbali za kazi kwa mwezi Septemba 2024. Kampuni hii inajivunia kutoa huduma bora za usafiri wa anga, na sasa inapanua wigo wake kwa kuongeza idadi ya wafanyakazi wenye ujuzi na sifa za kipekee katika sekta ya usafiri wa anga.

Fursa Mpya za Ajira Air Tanzania Septemba 2024

Nafasi za Kazi Zilizotangazwa

  1. Foreign Captain – Nafasi 10

    • Mahali: Dar es Salaam, Tanzania
    • Sifa za Mwombaji:
      • Leseni ya Pilot wa Usafiri wa Ndege (Airline Transport Pilot License) na Uzoefu wa zaidi ya masaa 3500 ya urushaji ndege.
      • Uzoefu wa saa 1000 kama rubani mkuu (Pilot in Command) na uzoefu wa kuendesha ndege zenye uzito wa tani 20 au zaidi.
      • Leseni halali, na uzoefu wa masaa 500 kama rubani mkuu kwenye aina za ndege kama B787, B737MAX, Q400, au Q300.
    • Majukumu:
      • Kusimamia usalama wa ndege na abiria wake kabla, wakati na baada ya safari.
      • Kuripoti matukio na ajali zozote zinazoweza kutokea.
      • Kuhakikisha mipango ya safari za ndege na nyaraka zote muhimu zipo sahihi na salama.
    • Mkataba: Mwaka 1, na malipo mazuri pamoja na marupurupu.
  2. Captain – Nafasi 30

    • Mahali: Dar es Salaam, Tanzania
    • Sifa za Mwombaji:
      • Uzoefu wa zaidi ya masaa 3500 ya urushaji ndege na leseni ya Pilot wa Usafiri wa Ndege (Airline Transport Pilot License).
      • Uzoefu wa saa 1000 kama rubani mkuu na uwezo wa kuendesha ndege zenye uzito wa tani 20 au zaidi.
    • Majukumu:
      • Kusimamia usalama wa ndege, abiria, na mizigo kabla, wakati na baada ya safari.
      • Kuwa na nidhamu ya hali ya juu na kuhakikisha usafi na ulinganifu wa mavazi ya timu nzima ya usafiri.
    • Mkataba: Miaka 10 kwa watanzania, na malipo mazuri pamoja na marupurupu.
  3. First Officer – Nafasi 4

    • Mahali: Dar es Salaam, Tanzania
    • Sifa za Mwombaji:
      • Leseni ya rubani wa biashara (Commercial Pilot License) na uzoefu wa zaidi ya masaa 250 ya urushaji ndege.
      • Uwezo wa kushiriki katika mipango ya safari na kuhakikisha usalama wa safari nzima.
    • Majukumu:
      • Kutoa msaada kwa rubani mkuu katika shughuli zote za urushaji ndege, ikiwa ni pamoja na kuhakikisha urambazaji sahihi wa ndege.
    • Mkataba: Miaka 10, na malipo mazuri pamoja na marupurupu.
  4. Public Relations Officer II – Nafasi 1

    • Mahali: Dar es Salaam, Tanzania
    • Sifa za Mwombaji:
      • Shahada katika fani ya Mahusiano ya Umma, Mawasiliano ya Biashara, Uandishi wa Habari au kiwango cha sawa kutoka taasisi inayotambulika.
    • Majukumu:
      • Kusimamia maudhui ya kidijitali na kufanya kazi za mahusiano ya umma, kama vile kuandika makala na kuandaa taarifa kwa vyombo vya habari.
      • Kusimamia shughuli zote za mawasiliano na habari kuhusu Air Tanzania.
    • Mkataba: Miaka 10, na malipo mazuri pamoja na marupurupu.

Jinsi ya Kuomba:

Wale walio na sifa zinazohitajika wanakaribishwa kutuma maombi yao kupitia ATCL Recruitment Portal kwa kutumia anwani: recruitment.atcl.co.tz. Barua ya maombi inapaswa kuelekezwa kwa Mkurugenzi Mtendaji & CEO wa Air Tanzania. Mwisho wa kutuma maombi ni siku 14 tangu tarehe ya tangazo hili.

Bofya Hapa Kupakua Tangazo la Ajira Air Tanzania Septemba 2024

Mapendekezo ya Mhariri:

  1. Nafasi Mpya za Kazi Amana Bank September 2024
  2. Nafasi 2 za Msimamizi wa Malipo ya Miwa Kilombero Sugar Co. Ltd August 2024
  3. Nafasi za Mwakilishi Mauzo (Sales Representative) Kilombero Sugar Co. Ltd – Agosti 2024