Ratiba ya Ligi Kuu NBC Tanzania Bara 2024/2025 | Msimu wa 2024-2025 wa Ligi Kuu Tanzania Bara, maarufu kwa jina la Ligi Kuu ya NBC 2024/2025, unatarajiwa kuanza kwa kishindo Agosti 16, 2024. Msimu huu unatarajiwa kuwa wa kusisimua zaidi huku timu 16 zikiwa zimechuana vikali kuwania ubingwa.
Bodi ya Ligi Kuu Tanzania Bara (TPL) imetangaza rasmi kuanza kwa msimu mpya wa 2024-25 wa Ligi Kuu Tanzania Bara unaotarajiwa kuanza kutimua vumbi Agosti 16, 2024.
Ratiba ya Ligi Kuu NBC Tanzania Bara 2024/2025, Msimu huu unatarajiwa kuwa na ushindani wa hali ya juu kutokana na maboresho yaliyofanywa kwenye vikosi vya timu kadhaa ambazo zote zimeonyesha wazi nia ya kutaka kuipa changamoto Yanga Sc kutetea ubingwa wao.
Kabla ya kuanza kwa Ligi Kuu, mashabiki wa soka watashuhudia mechi ya Ngao ya Jamii, itakayochezwa kati ya tarehe 8 na 11 Agosti 2024. Mechi hii ya jadi itakuwa kipimo cha awali cha uwezo wa timu kabla ya kuanza kwa msimu rasmi/Ratiba ya Ligi Kuu NBC Tanzania Bara 2024/2025.
Ratiba ya Ligi Kuu NBC Tanzania Bara 2024/2025
Msimu wa Ligi Kuu ya 2024/2025 utakuwa na raundi 30, ambapo kila timu itacheza dhidi ya nyingine mara mbili, nyumbani na ugenini. Msimu unatarajiwa kumalizika tarehe 24 Mei 2025, na kutakuwa na dirisha dogo la uhamisho lililofunguliwa kuanzia tarehe 15 Desemba 2024 hadi Januari 15, 2025, ambapo timu zitapata fursa ya kuimarisha vikosi vyao/Ratiba ya Ligi Kuu NBC Tanzania Bara 2024/2025.
Mei 5, 2025
🕓 4:00 jioni
JKT Tanzania vs Simba SC
Uwanja: Isamuyo Stadium
Mei 8, 2025
🕓 4:00 jioni
Simba SC vs Pamba Jiji
Uwanja: KMC
Mei 11, 2025
🕓 4:00 jioni
KMC FC vs Simba SC
Uwanja: KMC Complex
Mei 12, 2025
🕓 4:00 jioni
Tanzania Prisons vs Coastal Union
🕡 6:30 jioni
Kagera Sugar vs Mashujaa FC
Mei 13, 2025
🕑 2:00 mchana
JKT Tanzania vs Fountain Gate
🕟 4:15 jioni
Kengold FC vs Pamba Jiji
🕟 4:15 jioni
Young Africans vs Namungo FC
🕖 7:00 usiku
Azam FC vs Dodoma Jiji
Mei 14, 2025
🕓 4:00 jioni
Simba SC vs Singida BS

Yanga SC ambao ni mabingwa watetezi wa msimu wa 2023-2024 watakuwa na kibarua cha kutetea ubingwa wao dhidi ya timu nyingine kali. Msimu huu, Ligi Kuu itawakaribisha wapya Kengold FC kutoka Tukuyu, Mbeya, na Pamba Jiji FC ya Mwanza, ambazo zote zimepanda daraja kutoka Daraja la Kwanza/Ratiba ya Ligi Kuu NBC Tanzania Bara 2024/2025.
Hii hapa Ratiba ya Ligi Kuu NBC Tanzania Bara 2024/2025 kama ilivyo kwenye jedwali hapo chini:-
CHECK ALSO:
Weka maoni yako