Singida Black Stars Wamtaka Amankona, Kuimarisha Safu ya Ushambuliaji | Klabu ya Singida Black Stars ya Tanzania imeonyesha nia ya kutaka kumsajili mshambuliaji mahiri Mghana Stephen Amankona (25) mchezaji wa Berekum Chelsea.
Habari za uhakika zimeeleza kuwa mazungumzo baina ya pande hizo mbili yanaendelea, na tayari mchezaji huyo ametajwa kuwa nyota wa Singida Black Stars kwa msimu wa 2025/2026.
Singida Black Stars Wamtaka Amankona, Kuimarisha Safu ya Ushambuliaji
Stephen Amankona ni mchezaji mwenye uwezo mkubwa wa kufumania nyavu, akiwa ameibuka mfungaji bora wa Ligi Kuu Ghana kwa misimu miwili mfululizo:
Msimu wa 2024/25: Mabao 15
Msimu wa 2023/24: Mabao 19
Uwezo wake wa kuongoza mashambulizi umemfanya alengwe na klabu kadhaa za Afrika. Singida Black Stars inaamini kusajiliwa kwake kutaimarisha kwa kiasi kikubwa kikosi chao hasa katika mashindano ya ndani na nje ya nchi.
CHECK ALSO:
Weka maoni yako