Usajili Yanga Leo, Wachezaji Wanaotakiwa na Wananchi | TETESI ZA USAJILI YANGA, Klabu ya Yanga SC ambayo ni moja ya klabu kongwe na yenye mafanikio makubwa katika historia ya soka la Tanzania, imeanza rasmi maandalizi ya msimu mpya wa 2025/2026 kupitia usajili wa kimkakati. Usajili huu unalenga kuimarisha kikosi kwa ajili ya mashindano ya kitaifa na kimataifa, kama vile Ligi Kuu ya NBC, Kombe la Shirikisho la CRDB, na michuano ya CAF.
Katika mchakato huu wa usajili, uongozi wa klabu hiyo unaendelea kuwachambua kwa makini wachezaji wenye uwezo wa kuongeza ushindani wa kikosi hicho, huku ukizingatia pia vigezo vya kiufundi vilivyowekwa na wakufunzi. Wachezaji wapya waliosajiliwa wanatarajiwa kuwa na uzoefu, nidhamu, na uwezo wa kucheza kwa kiwango cha juu katika mazingira yenye ushindani mkubwa.
Usajili Yanga Leo, Wachezaji Wanaotakiwa na Wananchi
Yanga wamezamiria kufanya sajili zifuatazo ili kuimarisha kikosi chao kuelekea msimu wa 2025/2026, na kuongeza baadhi ya wachezaji wao mikataba ili kusalia katika kikosi chao:-
- 🇲🇱 Mkataba wa Djigui Diarra na YANGA SC 🇹🇿 unatarajiwa kuisha Juni 30.
- Wachezaji watatu wa Yanga SC 🇹🇿 watakaoongeza mikataba yao ya kusalia Yanga hadi Juni 2027.✅ 🇨🇩 Maxi Nzengeli
✅🇹🇿 Dickson Job
✅ 🇮🇪 Pacome Zouzoua - Jonathan Sowah kutoka Singida Black Stars
- Feisal Salum Fei toto kutoka Azam
- Ecua Celestin kutoka Zoman FC

Aidha, Yanga SC imejikita katika kusajili wachezaji wa kimataifa na ndani wenye vipaji vya kipekee ili kuhakikisha klabu hiyo inaendelea kupambana vikali na kulinda heshima yake katika ngazi ya kitaifa na kimataifa. Hii ni sehemu ya mkakati mpana wa kuimarisha kikosi, kuongeza ushindani wa nafasi, na kufikia malengo ya kutwaa mataji mengi msimu ujao.
Usajili huu wa msimu wa 2025/2026 unaonekana kuwa hatua muhimu kuelekea mafanikio makubwa kwa klabu hiyo, huku mashabiki na wadau wa soka wakisubiri kwa hamu kutangazwa kwa wachezaji wapya na mabadiliko yatakayofanyika ndani ya kikosi hicho.
CHECK ALSO:
Weka maoni yako